Uraia na Maadili Darasa la VI Syllabus

    1. Kujenga urafiki mwema na mataifa mengine
      1. Kuainisha uhusiano wa Tanzania na nchi nyingine
      2. Kutambua jumuiya za ushirikiano wa kimataifa
    2. Kuheshimu tofauti za kiutamaduni na mitazamo miongoni mwa watu wa jamii tofauti
      1. Kubainisha mikakati ya kukabiliana na athari za utandawazi
      2. Kueleza umuhimu wa kujenga umoja wa kitaifa katika jamii zenye tamaduni tofauti
      3. Kueleza njia za kujenga uhusiano mzuri baina ya watu wenye tamaduni tofauti
    3. Kucha ngamana na watu wenye asili tofauti
      1. Kueleza mipaka ya ushiriki wa watu wenye asili tofauti katika mambo ya kijamii
      2. Kueleza haki ya uhuru wa kuishi kwa raia yeyote nchini Tanzania
      3. Kufafanua umuhimu wa kudumisha uhusiano ya kibiashara, utamaduni na michezo kwa watu wa asili tofauti
    1. Kusimamia haki
      1. Kufafanua mihimili mitatu ya serikali
      2. Kutofautisha mamlaka na majukumu ya serikali ya Kijiji/Mtaa, Kata, Wilaya, Mkoa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
      3. Kushirikiana na vikundi vya kijamii kutetea haki za binadamu
      4. Kuelimisha watu wengine kuepuka mila na desturi zinazokiuka haki za binadamu
      5. Kuainisha mila na desturi zinazokiuka haki za binadamu
    2. Kutimiza majukumu yake kwa uwazi na ukweli
      1. Kufichua maovu yanayo husiana na ubadhirifu na ufisadi katika utekelezaji wa majukumu
      2. Kuonesha tabia ya kupiga vita unafiki katika maisha
      3. Kuthibitisha kauli ya ukweli kwa mifano dhahiri katika maisha ya kila siku
    3. Kuaminika katika jamii
      1. Kuonesha tabia ya kujiepusha na matendo yenye kuharibu mahusiano mazuri baina ya watu
      2. Kutathmini utekelezaji wa wajibu wake
    1. Kujifunza kwa kuchanganua mambo kiyakinifu
      1. Kuonesha tabia ya ushirikiano na watu wengine katika kujifunza
      2. Kutathmini uwezo wake katika kujifunza na kuboresha utendaji
      3. Kudadisi na kujifunza kwa kutumia mazingira
    2. Kufikia malengo aliyojiwekea kwa kuwa na mtazamo chanya
      1. Kuboresha utendaji katika kufikia malengo aliyojiwekea
      2. Kuonesha tabia ya kujifunza na kutenda kwa kutumia uzoefu wa wengine katika kufikia malengo
      3. Kupanga mpango mkakatiunao tekelezeka katika kufikia malengo
      4. Kuonesha tabia ya uthubutu katika kufikia malengo aliyojiwekea
    3. Kuvumilia katika maisha ya kila siku
      1. Kuonesha tabia ya kuishi kwa matumaini na kukiri ushindi dhidi ya mabadiliko
      2. Kuhamasisha wengine kukabiliana na changamoto za kimaisha kwa kutumia uzoefu wake
      3. Kufanya matendo yaliyo ndani ya uwezo wake kuhimili changamoto inayomkabili
    1. Kushirikiana katika kutekeleza majukumu ya nyumbani na shuleni
      1. Kushirikiana na wanajamii katika shughuli za kimaendeleo
      2. Kutambua faida za kushirikisha watu wengine na hasara za kutoshirikisha wengine katika utekelezaji wa majukumu
    2. Kuwa na nidhamu binafsi
      1. Kufanya maamuzi kwa wakati katika kutekeleza majukumu
      2. Kutetea msimamo wake kwa hoja
      3. Kubainisha vipaumbele vyake katika masomo na kuvizingatia
    3. Kutii sheria na kanuni katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku
      1. Kutathmini hatua zinazo chukuliwa kudhibiti uvunjifu wa sheria na kanuni shuleni
      2. Kuhoji sheria na kanuni zinazotumika
      3. Kuoanisha utekelezaji wa kanuni katika maisha
      4. Kutambua kanuni za nchi na kuzifuata
    4. Kusimamia majukumu yanayomhusu nyumbani na shuleni
      1. Kupendekeza njia za uboreshaji utendaji wa kazi
      2. Kubaini njia mbadala za kutatua matatizo
      3. Kutambua majukumu ya kiongozi katika ngazi ya shule na familia
    5. Kulinda rasilimali na maslahi ya nchi
      1. Kupambanua sifa za kiongozi anayefaa kuchaguliwa katika ngazi ya Taifa
      2. Kufanya vitendo vya kulinda usalama wa Taifa
      3. Kubaini njia za kupambana na matumizi mabaya ya mali ya umma
      4. Kutumia vipaji na uwezo wake kubuni shughuli zenye kuleta mae ndeleo
    1. Kujenga uhusiano mzuri na watu wengine katika jamii
      1. Kutatua migogoro miongoni mwa wanafunzi wenzake
      2. Kufanya vitendo vinavyo dumisha urafiki mwema na wenzake
      3. Kueleza vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa maelewano katika jamii
    2. Kutunza mazingira na vilivyomo
      1. Kukemea ukiukwaji wa kanuni zinazotunza mazingira
      2. Kufafanua njia bora za kuzuia uharibifu wa mazingira
    3. Kujijali na kuwajali wengine
      1. Kutenda matendo kwa kuzingatria usawa
      2. Kuwatanguliza watu wenye uhitaji wa haraka kupata huduma
      3. Kuomba ushauri pale inapohitajika
      4. Kufanya vitendo vinavyo wavutia wenzake kujiepusha na tabia hatarishi
      5. Kukemea vitendo vinavyoweza kuhatarisha ustawi wa jamii
    1. Kuipenda Tanzania kwa kuenzi tunu mbalimbali za nchi na asili yake
      1. Kufafanua utekelezaji wa demokrasia nchini
      2. Kueleza dhamira ya siku kuu za kitaifa.
      3. ubainisha muundo wa uongozi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
      4. Kueleza umuhimu wa tunu za Taifa
      5. Kufafanua njia mbalimbali za kuitangaza nchi yake ya Tanzania
    2. Kujipenda na kuwapenda watu wengine
      1. Kuonesha matendo mema na ya heshima
      2. Kuthamini mchango wa watu wengine katika ustawi wa jamii
      3. Kuonesha tabia ya kupenda kutoa msaada kwa watu wenye mahitaji mbalimbali
    3. Kuipenda na kujivunia shule yake
      1. Kutunga nyimbo/ ngonjera/ mashairi ya kuisifu shule yake
      2. Kueleza ujumbe uliomo katika kauli mbiu na wimbo wa shule yake