Kiswahili Darasa la V Syllabus

    1. Kusoma kwa ufasaha na kuonesha uelewa wa matini aliyoisoma
      1. Kueleza maana za maneno mapya katika matini mbalimbali, kuyatumia katika sentensi na kuhusianisha na mazingira ya kila siku
      2. Kubaini maudhui yaliyomo katika hadithi na kuelezea tabia zote za kila mhusika na kuhusianisha na mazingira ya kila siku
      3. Kusoma matini teule za kisiasa, kiuchumi na kijamii, kubaini maneno mapya na kuyatumia katika miktadha mbalimbali
      4. Kusoma, kuchanganua na kueleza mawazo yote ya msingi katika matini teule za kisiasa, kiuchumi na kijamii
      5. Kusoma matini teule kwa kuzingatia alama zote za uandishi na kuelezea umuhimu wa matini hizo
    2. Kutumia msamiati katika kusoma ili kuchanganua mawazo yaliyo wasilishwa katika matini mbalimbali
      1. Kusoma kifungu cha habari ili kubaini maneno mapya yenye maana zaidi ya moja
      2. Kusoma matini mbalimbali yanayoelezea hali ya hewa na kubaini majira yake
      3. Kusoma matini na kubaini maneno mapya na kuelezea maana zake
    3. Kusikiliza na kuonesha uelewa wa jambo alilosikiliza
      1. Kusoma hotuba na kubaini maudhui yaliyojitokeza na kuyafafanua kwa usahihi
    4. Kusoma kwa ufasaha na kuonesha uelewa wa matini mbalimbali
      1. Kusoma kitabu cha hadithi na kuelezea tabia za wahusika
      2. Kusoma hadithi za kubuni kwa burudani na kwa kuzingatia alama za uandishi
      3. Kusoma matangazo na kubaini taarifa muhimu
      4. Kubaini makosa ya kiuandishi katika matini anuai
      5. Kusoma na kubaini methali zinazofanana
      6. Kusoma methali mbalimbali katika kifungu cha habari na kueleza maana zake
    5. Kusikiliza na kuonesha uelewa juu ya jambo alilolisikiliza
      1. Kubaini na kuchambua hoja kuu zilizotolewa katika majadiliano
      2. Kubaini mawazo makuu katika risala
      3. Kubaini miundo katika sentensi wakati wa mazungumzo
      4. Kusikiliza habari na kujibu maswali yatokanayo na habari