Kiswahili (New) Form 3 Syllabus

    1. Kukuza uelewa wa sarufi ya Kiswahili
      1. Kuunda maneno kwa njia mbalimbali kutokana na habari alizozisoma au kuzisikiliza (mf. utohoaji, uradidi, uhulutishaji)
      2. Kuandika habari kwa kuzingatia maneno yaliyoundwa kwa njia mbalimbali
      3. Kujenga hoja za uga mahususi kwa kutumia miundo mbalimbali ya sentensi (mf. siasa, uchumi, kilimo na biashara)
      4. Kuandika matini ndefu na changamani kwa kutumia miundo mbalimbali ya sentensi
    1. Kusikiliza na kuelewa mazungumzo
      1. Kusikiliza habari changamani kitunduizi na kuchangia au kutoa maoni mwafaka
      2. Kusikiliza habari na kuzielezea kwa maneno yake mwenyewe kwa kuzingatia stadi za mawasiliano (mf. uwazi, ukamilifu wa hoja, usahihi, muwala, uwekevu na staha)
    2. Kusoma matini kwa ufasaha na ufahamu
      1. Kusoma matini ndefu changamani na kuelezea kwa maandishi mawazo makuu yaliyomo kwa kuzingatia stadi za mawasiliano (mf. uwazi, ukamilifu wa hoja, usahihi, muwala, uwekevu na staha
      2. Kusoma matini ndefu changamani na kutathmini hoja zilizomo
    1. Kuwasiliana kwa ufasaha kwa njia ya mazungumzo
      1. Kutumia lugha fasaha katika mazungumzo ya hadhara (mf. mikutano ya hadhara, uwasilishaji mbele ya halaiki na mijadala mbalimbali)
    2. Kuwasiliana kwa njia ya maandishi katika miktadha mbalimbali
      1. Kuandika barua na makala za magazetini
    1. Kukuza uelewa wa misingi ya fasihi ya Kiswahili
      1. Kufafanua dhana ya fasihi na fasihi ya Kiswahili (maana, aina na dhima)
      2. Kuchambua tanzu za fasihi simulizi na andishi
    2. Kuhakiki kazi za fasihi ya Kiswahili
      1. Kujadili dhana ya uhakiki wa kazi za fasihi (maana ya uhakiki, mhakiki na sifa za mhakiki)
      2. Kufafanua misingi ya uhakiki wa kazi za fasihi simulizi na fasihi andishi (vipengele vya fani na maudhui)
      3. Kuhakiki fani na maudhui katika kazi za fasihi simulizi (mashairi na maigizo)
      4. Kuhakiki fani na maudhui katika tamthiliya
      5. Kutathmini namna maudhui ya kazi alizozihakiki yanavyosadifu jamii inayomzunguka
    3. Kubuni kazi za fasihi ya Kiswahili
      1. Kujadili kanuni za utunzi wa nyimbo, ngonjera na maigizo
      2. Kutunga nyimbo, ngonjera na maigizo
      3. Kuimba nyimbo na kutamba ngonjera
      4. Kuigiza maigizo
    1. Kufanya tafsiri sahili katika lugha ya Kiswahili
      1. Kujadili dhana, misingi, kanuni, na hatua za tafsiri
      2. Kutafsiri matini fupi sahili
      3. Kutatua changamoto zinazojitokeza katika kutafsiri matini
    2. Kuhariri matini mbalimbali za Kiswahili
      1. Kujadili dhana, kanuni na misingi ya uhariri
      2. Kuhariri matini fupi za Kiswahili