Kiswahili Darasa la VII Syllabus

    1. Kutumia msamiati katika kuandaa matini mbalimbali
      1. Kufupisha habari/hadithi aliyoisoma kwa kutumia maneno yake na kubainisha mawazo yote ya msingi ya mwandishi na kuyaelezea kwa usahihi
      2. Kusikiliza hotuba na kubainisha mambo muhimu yanayotokana na hotuba na kuyahusianisha na maisha ya kila siku
      3. Kuandika insha inayoeleweka kuhusu uharibifu wa mazingira kwa kuzingatia alama zote za uandishi
      4. Kutunga hadithi fupi na kuelezea maana za maneno yote mapya na kuelezea jinsi yanavyotumika katika maisha ya kila siku
    2. Kutumia msamiati katika kuandaa matini mbalimbali
      1. Kuandika shairi linaloelezea muonekano wa hali ya hewa katika mazingira kwa kuzingatia kanuni za shairi
      2. Kuandika habari fupi kwa kutumia majina sahihi ya kazi za watu
      3. Kuandika sentensi kwa kutumia maneno yanayoonesha umiliki
    3. Kutumia msamiati katika uandishi katika kuandaa matini mbalimbali
      1. Kuunda maneno mapya kwa kubadili mpangilio wa herufi na silabi (mila-lami, lima, mali) ili kukuza msamiati
      2. Kuchanganua vitu mbalimbali na kuvitofautisha kiasi chake katika sentensi kwa kutumia ….ingi.… ....engi….. …kidogo…… ....chache.......
      3. Kuandika insha yenye kueleweka kuhusu ugonjwa wa UKIMWI
      4. Kuandika kifungu cha habari fupi kwa mpangilio wa sentensi unaoeleweka
    4. Kutumia msamiati katika uandishi wa matini mbalimbali
      1. Kuandika hadithi fupi kwa kuzingatia kanuni na alama za uandishi
      2. Kuandika habari fupi kwa mpangilio unaoeleweka kuhusu shughuli za kila siku
    5. Kuandika sentensi kwa kutumia nyakati mbalimbali (uliopo, ujao uliopita na timilifu)
    6. Kutumia maandishi katika mawasiliano kulingana na miktadha mbalimbali
      1. Kubaini muundo wa kadi za mialiko, kuandika na kueleza matumizi yake
      2. Kueleza kanuni za uandishi wa baruayakirafiki na rasmi, kutaja faida zake na kueleza namna ya kuzitumia barua hizo katika mazingira ya kila siku
      3. Kubaini miundo ya barua za kirafikinarasmi na kuiandika kwa kuitofautisha katika miktadha mbalimbali
    7. Kutumia maandishi katika kuwasiliana kulingana na miktadha mbalimbali
      1. Kuandika hadithi fupi yenye maana kwa kuzingatia alama za uandishi na mtiririko wa matukio katika aya
      2. Kuandika Insha kimantiki kuhusu elimu ya afya na uzazi
      3. Kuandika majina ya ndege waliopo katika mazingira yao na kuelezea sifa na tabia zao
      4. Kuandika barua ya kiofisi kwa kuzingatia mtiririko wa vipengele vya uandishi wa barua
      5. Kuandika habari kwa kuzingatia taratibu na alama za uandishi
      6. Kuandika risala fupi kwa kuzingatia muundo na kanuni za uandishi
      7. Kuandika insha kuhusu umuhimu wa kuwa na familia ndogo
      8. Kuandika kumbukumbu za mikutano kwa kuzingatia vipengele vyake vya uandishi
      9. Kuandika methali zenye mafunzo kulingana na kifungu cha habari
      10. Kuandika vipengele vya muundo wa insha
      11. Kufupisha habari katika maandishi bila kupotosha maana iliyokusudiwa na kwa kuzingatia alama za uandishi
      12. Kuandika kirefu cha vifupisho vya maneno au majina ya msingi (JKT, UDA, TBC TET, BMT)
      13. Kuandika matangazo mbalimbali kuzingatia kwa taratibu za uandishi
    8. Kutumia msamiati katika kuzungumza kwa kuwasilisha hoja kulingana na miktadha mbalimbali
      1. Kusoma habari na kubainisha maneno mapya na kuelezea maana zake kwa kutumia kamusi
      2. Kuelezea na kubaini maneno mapya katika risala iliyowasilishwa
      3. Kubaini aina saba za maneno katika sentensi (Nomino, kitenzi, kielezi, kivumishi, kiwakilishi, kiunganishi na kihisishi)
    9. Kutumia msamiati katika kuzungumza kwa kuwasilisha hoja kulingana na muktadha mbalimbali
      1. Kuelezea idadi ya vitu vinavyohesabika katika umoja na wingi kwa kutumia sentensi kanushi
      2. Kutofautisha na kueleza vitu katika hali ya ukubwa na udogo wake
      3. Kuelezea muonekano wa hali ya hewa katika mazingira yake kikamilifu (ukungu, upepo, joto, baridi, mvua)
      4. Kuelezea shughuli anazotenda mwanafunzi kila siku shuleni na kuandika habari fupi kwa mpangilio
      5. Kuelezea shughuli za mwanafunzi anazotenda kila siku nyumbani kwa mpangilio
      6. Kufanya ziara nje ya darasa na kubaini majina ya maua tofauti yanayopatikana na kuelezea sifa zake
      7. Kusimulia hadithi fupi kwa kutumia majina ya wanyama wa porini
      8. Kutunga sentensi kwa kutumia majina ya wanyama wanaofugwa na kuelezea faida zake
    10. Kutumia msamiati katika mazungumzo kwa kuwasilisha hoja kulingana na miktadha mbalimbali
      1. Kusoma magazeti mbalimbali yanayoelezea shughuli za kielimu, kiuchumi na kisiasa na kubaini maneno mapya, kuelezea maana zake na kuyatungia sentensi kwa usahihi
      2. Kuandika risala kwa kuzingatia alama za uandishi na kuelezea matumizi yake katika miktadha mbalimbali
      3. Kubainisha na kuelezea mambo muhimu ya kuzingatia katika uandishi wa risala na kueleza matumizi yake kwa usahihi kwa kuzingatia miktadha mbalimbali
      4. Kutunga hadithi fupi na kuelezea mafunzo yanayopatikana katika hadithi hiyo na kuhusianisha na maisha ya kila siku
      5. Kutunga sentensi kwa kutumia aina saba za maneno kwa usahihi kwa kuzingatia miktadha mbalimbali
      6. Kubainisha aina saba za maneno na dhima zake katika sentensi na kutambua kifupisho cha kila aina ya neno
      7. Kuwasilisha hoja na kuzielezea kwa kufuata mpangilio sahihi wa mawazo katika miktadha mbalimbali
    11. Kutumia msamiati katika kuanzisha na kuendeleza mazungumzo katika miktadha mbalimbali
      1. Kubainisha majina ya wanyama, muonekano, sauti zao na kueleza wanakoishi
      2. Kutaja majina ya wanafamilia nyumbani katika kusimulia hadithi fupi na kubainisha uhusiano wao
    12. Kuanzisha na kuendeleza mazungumzo katika miktadha mbalimbali
      1. za nahau na kutumia nahau mbalimbali katika mazungumzo kwa kuzingatia miktadha mbalimbali
      2. Kutumia nafsi tatu katika sentensi kwa kuzingatia hali ya umoja na wingi
      3. Kutoa taarifa kwa ukamilifu kuhusu tukio lililotokea
      4. Kushiriki katika mjadala kuhusu matumizi ya simu ya mdomo
      5. Kueleza hatua za uandishi wa habari fupi/ insha
      6. Kueleza mafunzo yaliyopatikana katika methali na kulinganisha na maisha ya kila siku katika miktadha mbalimbali
      7. Kusimulia mambo yaliyoonekana baada ya kufanya ziara fupi katika mazingira ya jirani na shule
      8. Kusimulia hadithi kwa kuzingatia mtiririko wa mawazo
      9. Kutafsiri lugha ya picha katika vitendawili na kuelezea maana zake kwa kuhusianisha na maisha ya kila siku
      10. Kutunga sentensi kwa kutumia kauli taarifa
      11. Kutumia nahau katika sentensi mbalimbali
      12. Kubainisha na kueleza taswira za kimawazo zilizo katika nahau kutoka katika hadithi
      13. Kusimulia hadithi yenye methali na kuelezea maana ya mafunzo yaliyopatikana katika methali
      14. Kuchambua maudhui yote yaliyomo katika mashairi ya kimapokeo na kisasa, kuyaelezea na kuyahusianisha na mazingira ya kila siku
      15. Kutunga sentensi kwa kutumia kauli halisi
      16. Kutambua methali zinavyotumika katika mazungumzo na kuelezea maana zake
      17. Kutafsiri taswira inayoakisiwa na nahau
      18. Kughani tenzi na kuelezea ujumbe unaopatikana na kuhusianisha na mazingira ya kila siku
      19. Kuelezea vitu vilivyopo katika mazingira yao katika hali ya umoja na wingi kwa vitu vyenye uhai na visivyo na uhai
      20. Kuigiza igizo dhima kuhusu elimu ya biashara na kueleza umuhimu wake
      21. Kughani shairi kwa kuzingatia kanuni za mashairi (vina, mizani na kituo)
      22. Kutumia nahau katika habari fupi na kuelezea maana zake
      23. Kutunga mashairi ya kisasa yenye beti sita au zaidi na kuyahusianisha na mazingira ya kila siku
      24. Kutaja na Kueleza mawazo makuu yaliyomo katika wimbo wa kizalendo
      25. Kutamba ngonjera kwa kuzingatia kanuni za utambaji
      26. Kutunga mashairi ya kimapokeo yenye mishororo minne kwa kuzingatia kanuni za utunzi wa mashairi na kuyahusianisha na mazingira ya kila siku
      27. Kutega na kutegua vitendawili na kuvihusianisha na vitu vilivyopo katika mazingira kwa usahihi
      28. Kubainisha na kueleza sifa za mashairi ya kimapokeo na kisasa na kuyatofautisha
      29. Kuimba wimbo wa kizalendo kwa ufasaha (Tazama Ramani)
    13. Kutumia matamshi sahihi katika kutamka maneno mbalimbali
      1. Kutamka matamshi sahihi ya maneno yenye herufi ‘l’ na ‘r’
      2. Kutamka maneno yenye herufi ‘z’ na ‘dh’
      3. Kutamka maneno yenye herufi ‘s’ na ‘th’ kwa usahihi
    14. Kutambua sauti mbalimbali katika matamshi ya silabi, maneno sentensi na habari fupi
      1. Kutamka sauti za herufi mwambatano ng’w, nyw, shw na nyingine zenye muundo huo katika silabi, sentensi, maneno na habari fupi
      2. Kutamka sauti za herufi mwambatano lw, pw, sw, tw na nyingine zenye muundo huo katika silabi, maneno, sentensi na habari fupi
      3. Kutamka sauti za herufi mwambatano gh, py, nz, ky na herufi nyingine zenye muundo huo katika silabi, maneno, sentensi na habari fupi