Historia ya Tanzania na Maadili (New) Form 2 Syllabus

    1. Kutumia maarifa na ujuzi wa chimbuko na ukuaji wa mfumo wa ukoloni kuelewa uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na mataifa yaliyoitawala
      1. Kuchambua chimbuko la ukoloni
      2. Kubainisha mataifa yaliyoitawala Tanzania na mifumo yake ya kikoloni katika uchumi, utawala na utamaduni
      3. Kujadili mchango wa mifumo ya kikoloni katika uhusiano wa Tanzania na mataifa yaliyoitawala
    2. Kutathmini athari za mfumo wa ukoloni kwenye maadili ya jamii za Kitanzania
      1. Kueleza hali ya maadili ya jamii za Kitanzania kipindi ukoloni unaingia
      2. Kuchambua athari za mfumo wa ukoloni katika maadili ya jamii za Kitanzania
      3. Kubaini maadili yaliyo- dumishwa na jamii za Kitanzania wakati wa ukoloni
    3. Kuchambua jitihada za jamii za Kitanzania kupinga ukoloni na maadili ya kikoloni
      1. Kubaini sababu za jamii za Kitanzania kupinga uvamizi wa kikoloni, ukoloni na maadili yake
      2. Kujadili njia mbalimbali zilizotumika na jamii za Kitanzania kupinga uvamizi wa kikoloni, ukoloni na maadili yake
      3. Kufafanua misingi na mbinu zilizotumika kupigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
      4. Kutathmini mchango wa harakati za kupinga uvamizi na ukoloni katika kutunza maadili ya Kitanzania na kujenga uzalendo
    1. Kuchambua mifumo ya uchumi, siasa, utamaduni, jamii na maadili iliyojengwa, 1961-1966
      1. Kueleza hali ya uchumi, siasa, utamaduni, jamii na maadili mara baada ya uhuru
      2. Kutathmini mikakati na changamoto za ujenzi wa Taifa kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni, kijamii na kimaadili kipindi cha 1961-1966
    2. Kumudu historia ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
      1. Kueleza chimbuko la Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
      2. Kubaini mchango wa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika kujenga umoja, mshikamano na maadili miongoni mwa Wazanzibari