Kiswahili (New) Form 1 Syllabus

    1. Kutambua Kiswahili kama kielelezo cha utaifa na utambulisho wa Mtanzania
      1. Kutumia Kiswahili katika mijadala mbalimbali kwa kuzingatia utamaduni wa Mtanzania (mf. matumizi ya tafsida na uteuzi wa maneno kulingana na mila na desturi za Mtanzania)
    2. Kukuza uelewa wa sarufi ya Kiswahili
      1. Kusimulia habari na matukio kwa kuzingatia kiimbo, mkazo, na lafudhi pamoja na dhima zake
      2. Kuandika hadithi kwa kuzingatia mpangilio na uhusiano sahihi wa maneno (nomino, vivumishi, vielezi, viwakilishi, vitenzi, vihisishi, vihusishi na viunganishi) katika sentensi
      3. Kuandika hadithi kwa kuzingatia mpangilio na uhusiano sahihi wa sentensi katika aya
    1. Kusikiliza na kuelewa mazungumzo
      1. Kusikiliza mazungumzo changamani na kujibu maswali
      2. Kueleza kwa muhtasari mazungumzo changamani aliyoyasikiliza
      3. Kushiriki katika majadiliano ya masuala mbalimbali kwa kuzingatia sifa za lugha ya mazungumzo (mf. lugha ya mkato, kupeana nafasi)
    2. Kusoma matini kwa ufasaha na ufahamu
      1. Kusoma matini fupi changamani kwa kuzingatia alama za uandishi, kasi sahihi na kiimbo cha tungo
      2. Kueleza namna alama za uandishi na kiimbo vinavyoathiri ujumbe katika usomaji wa matini fupi changamani
      3. Kuandika hoja kuu kutoka katika matini fupi changamani alizozisoma kwa kuzingatia sifa za lugha ya maandishi (mf. alama za uandishi, miunganiko sahihi ya tungo, usanifu)
      4. Kutumia TEHAMA kutafuta maana ya maneno mapya kutoka katika matini aliyoisoma
    1. Kutumia kamusi katika miktadha mbalimbali
      1. Kutumia msamiati kwa usahihi katika mazungumzo na maandishi
      2. Kutumia taarifa mbalimbali za kamusi katika mawasiliano ya mazungumzo na maandishi
    2. Kuwasiliana kwa ufasaha kwa njia ya mazungumzo
      1. Kuzungumza kwa ufasaha katika miktadha mbalimbali (mf. nyumbani, shuleni na hospitalini)
      2. Kutumia lugha kwa ufasaha katika malumbano ya hoja
    3. Kuwasiliana kwa njia ya maandishi katika miktadha mbalimbali
      1. Kujieleza kwa ufasaha kwa maandishi katika miktadha mbalimbali